ดาวน์โหลดและฟังเพลง Isaya 49: 14-16 พร้อมเนื้อเพลงจาก Pastor Abiudi Misholi

ฟังเพลงIsaya 49: 14-16

Pastor Abiudi Misholi30 เม.ย. 2013

เนื้อเพลง Isaya 49: 14-16

Isaya 49: 14-16 - Pastor Abiudi Misholi

Nasoma katika kitabu cha Isaya 49 na

Ule mstari wa 14 hadi wa 16 Biblia inasema hivi

Sayuni alisema Yehova ameniacha

Bwana amenisahau

Je mwanamke aweza kumsahau mtoto wake anyonyae

Hata asimuhurumie mwana wa tumbo lake

Naam hawa waweza kusahau

Lakini mimi sitakusahau wewe

Tazama nalikuchora katika vitanga

Vya mikono yangu na kuta zako ziko mbele zangu daima

Ndugu msikilizaji nataka nikwambie siku

Ya leo iko sauti ambayo imeongea masikioni mwako

Ya kwamba Mungu amekuacha na tena

Amekusahau na wala hajakuona

Hata mimi nimeshawahi kupita katika kipindi hichi

Nikaona kwamba Mungu ameniacha tena

Mungu amenisahau

Hata nikatamani nijitupie kwenye gari nigongwe nife

Lakini ikaja sauti nyingine kusema ya kwamba

Mungu hajanisahau tena Mungu hajanicha na

Mungu yuko pamoja nami

Ngoja nikwambie neno la leo

Sayuni wakalalamika

Wakasema Bwana umetuacha na Yehova ametusahau

Mungu akawauliza swali moja

Je mwanamke anaweza

Akamsahau mtoto wake anyonyaye asimuhurumie mwana

Wa tumbo lake

Lakini Mungu akajibu ilo swali tena yeye mwenyewe

Akasema mwanamke anaweza akamsahau mtoto wake

Lakini mimi sitakusahau wewe

Maana nimekuchora katika vitanga vya mikono

Yangu na kuta zako ziko mbele yangu daima

Wanawake wengi leo hii

Wanazaa watoto wao wanawatupa kwenye majalala

Wengine wanazaa watoto wao wanawauwa kwa siri

Wengine wanawatupa katika mashimo ya choo

Lakini Mungu anasema hawezi kukusahau wewe

Wengine wakawazaa watoto wao wakawapeleka kwa bibi zao

Hata misaada hawapeleki

Maana wamewasahau

Lakini Mungu anasema hawezi kukusahau wewe

Hawezi kusahau kazi yako

Hawezi kusahau watoto wako

Hawezi kusahau uaminifu wako

Ondoa ilo wazo la sikio la pili

Ambalo linasema Mungu amekusahau

Ilo linatoka kwa shetani wala halitoki kwa Mungu

Lakini Mungu anasema leo hawezi kukusahau wewe

Hawezi kukusahau mama yangu

Hawezi kukusahau baba Yangu

Hawezi kukusahau kijana

Hawezi kukusahau dada

Amekuchora katika mikono yake na kuta zako ziko mbele yake daima

Ebu weka mkono wako sasa mahali panapouma ukiwa

Una shida yeyote inakusumbua weka mkono moyoni mwako

Iwe unamatatizo mbali mbali naenda kukuombea sasa

Katika jina la Yesu Kristo mwana wa

Mungu uliyeketi mahali pajuu palipoinuka

Naenda kinyume sasa na kazi za shetani

Nakwenda kinyume na nguvu za giza

Nakwenda kinyume sasa na mamteso yote yanayokusumbua

Nayaamuru yatokeee kwa Jina la

Yesu Mungu aliye hai

Nayaamuru yatoke yarudi huko yalikotoka

Ukawe mzima baba

Ukafanikiwe kwenye kazi zako

Ukafanikiwe kwenye ndoa yako

Ukafanikiwe kwenye shughuli zako

Ukafanikiwe kwenye vitu vyako na masomo yako

Mungu akukumbuke na akubariki nakutakia maisha mema

Katika jina la Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye hai

Ukawe mzima

Hutanisahau

Hutanisahau

Hutanisahau baba

Wewe Mungu wewe wa huruma

Hutanisahau hutanisahau

Hutanisahau hutanisahau

Yesu hutanisahau hutanisahau

Hutanisahau wewe Baba wewe

Wewe Mungu wa huruma

Hutanisahau Ninakuabudu Yesu ninakuabudu

Ninakuabudu ninakuabudu Yesu Nakuabudu Baba

Ninakuabudu ninaaakuabudu wewe Baba

Wewe Mungu wa Huruma wa huruma ninakuabudu

Ninakuabudu

Ninakuabudu tena Messiah Messiah

Ninakuabudu

Ah ah Nakuabuuuduu Yesu wee

Ninakuabudu Halelu halelu halelu

Haleluuu nakuabudu Baba

Ewe Mungu ewe Mungu wa huruma

Wa huruma ninakuabudu

Nakutakia maisha mema maisha ya amani na maisha ya furaha

Ubarikiwe na watoto wako ulindwe kazini mwako

Uinuliwe sana ufutwe machozi

Pokea haja ya Moyo wako kwa jina La Yesu Nakubariki

Amen

 

Amen

เกี่ยวกับเพลงนี้ :

เพลงนี้ถูกปล่อยออกมาในวันที่ 30 เม.ย. 2013, เพลง Isaya 49: 14-16 จาก Pastor Abiudi Misholi ที่ร่วมกันสร้างสรรค์ท่วงทำนองและเนื้อร้องได้ยอดเยี่ยม

ดาวน์โหลด JOOX Application และ รับฟังเพลง, ชมมิวสิควีดีโอ และอ่านเนื้อเพลง แบบออนไลน์ได้ทุกที่ทุกเวลา

Tags ที่เกี่ยวข้อง :

Isaya 49: 14-16 (โดย Pastor Abiudi Misholi), Isaya 49: 14-16, Isaya 49: 14-16 มิวสิควีดีโอ, Isaya 49: 14-16 เนื้อเพลง, Pastor Abiudi Misholi เพลง