Listen to Wana song with lyrics from Zuchu

Wana

Zuchu15 Apr 2020

Wana Lyrics

Wana - Zuchu

Lyrics by:Zuhura Soud

Composed by:Zuhura Soud

 

Hunywi maji yakapita

Mi nkiguna ushafika

Jina gani hujaniita baby

Ushauri hutaki kabisa

Eti uniache nna visa

Vya Firauni na Musa vingi

Nikilala naota kama unaniita

Nafumba macho navuta shuka

Naona napumbazika

Unishikapo ndipo hapo nafarijika

Mambo yako mahaba yako

Ndo maana natononoka weh

Wana wana wana wana

Pale tulipokutana

Mikono tukapeana

Macho yakatizamana

 

Wana wana wana wana

Pale tulipokutana

Namba kubadilishana

Nafsi kukubaliana aah

 

Nzi kidondani huvia

Wahenga walisema

Maradhi yaweza yasiwe na dawa

Kwa penzi yakapona

Rabii amenipa nusura

Jeuri sina tena

We ndo ganzi umenimaliza hasira

Siumwi wakisema

Nidekeze niliwaze

Washushuke wanyamaze

Nikinuna nibembeleze

Usinipepee nipulize

Watuone washituke

Roho zao ziwaume

Mi nipike ule chote

Unenepe upendeze

Wana wana wana wana

Pale tulipokutana

Mikono tukapeana

Macho yakatizamana

 

Wana wana wana wana

Pale tulipokutana

Namba kubadilishana

Nafsi kukubaliana aah mmh

Ukitaka uniweze nibebe wewe

Ukipenda unibimbe unikumbatie

Hata watu watuone wakahadithie

Nitambulishe niringe niwavimbie

Ukitaka uniweze nibebe wewe

Ukipenda unibimbe unikumbatie

Hata Lizer atuone akahadithie

 

Nitambulishe nitambe niwavimbie Wasafi

Popular Songs